Watoto watano kati ya nane wa familia moja wenye huko Chome Same wanahitaji masaada wa hali na mali ili waweze kuendesha maisha yao kutokana na ulemavu wa viungo walionao. Kutokana na maelezo ya mama mzazi Nirenjigwa Joseph watoto hao walizaliwa wazima ila walipata ulemavu baada ya kuanza kutembea. Baba wa watoto hao Amini Joseph Amini
alifariki mwaka 1992 baada ya hapo yeye amekuwa akilelea
familia hiyo.
Watoto hao Joseph Amini ( 38), Nafikahedi ( 33) ,Wediel (30) Gadison (28) na Julius (25) wote ni walemavu wa viungo ambao hutembea kwa kutambaa. Wanahitaji kuwa na mwangalizi wakati wote kwa hakuna wanaloweza kufanya bila usaidizi,
Kwa sasa ukiwaangalia watoto hao tayari wameshakuwa wakubwa kabisa na changamoto kubwa ni kwamba familia haiwezi kuwaacha kukaa pekee yao kwani wapo pia wa kike.Baada ya kutembelea familia hiyo waliona kuwa jamii hiyo inahitaji kusaidiwa kwani wanapoishi walemavu hao hakuna kivuli. Pia, wamekuwa wakitambaa kwenye jua na kusumbuliwa na tatizo la funza hivyo watasaidia kuweka baraza kwenye nyumba hiyo. Wamesema wataendelea kuhamasisha na jamii ili iisaidie familia hii.
Kwa mtu yeyote atakayeguswa kuweza kuisaidia familia hii anaweza kuwasiliana na Chediel Amini ambaye amebeba jukumu la kuwasaidia ndugu zake kwa simu namba 0654118385. Watoto hao Joseph Amini ( 38), Nafikahedi ( 33) ,Wediel (30) Gadison (28) na Julius (25) wote ni walemavu wa viungo ambao hutembea kwa kutambaa. Wanahitaji kuwa na mwangalizi wakati wote kwa hakuna wanaloweza kufanya bila usaidizi,
Kwa sasa ukiwaangalia watoto hao tayari wameshakuwa wakubwa kabisa na changamoto kubwa ni kwamba familia haiwezi kuwaacha kukaa pekee yao kwani wapo pia wa kike.Baada ya kutembelea familia hiyo waliona kuwa jamii hiyo inahitaji kusaidiwa kwani wanapoishi walemavu hao hakuna kivuli. Pia, wamekuwa wakitambaa kwenye jua na kusumbuliwa na tatizo la funza hivyo watasaidia kuweka baraza kwenye nyumba hiyo. Wamesema wataendelea kuhamasisha na jamii ili iisaidie familia hii.
No comments:
Post a Comment